.

Ijumaa, 11 Oktoba 2013

YANGA YATAMBA "TUTAIFUNGA SIMBA KIRAHISI KAMA KUMSUKUMA MLEVI TAREHE 20 OCT"

KOCHA Mkuu wa timu ya Yanga, Ernest Brandts, amesema kuifunga Simba katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom itakayochezwa Oktoba 20 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, ni kazi rahisi. Brandts amewatoa hofu viongozi na mashabiki wa Yanga, huku akitamba kupata ushindi dhidi ya mahasimu wao Simba. 

Akizungumza na RAI jana, Brandts alisema Simba hawamtishi kwa kuwa ana kikosi bora ambacho kina kila sababu ya kushinda mechi hiyo.

Alisema amekuwa akiifuatilia Simba mara nyingi inapocheza mechi na hakuna ushindani ambao umekuwa ukionyeshwa na wachezaji wa timu hiyo, licha ya kupata ushindi katika mechi zake.

“Simba hawana kiwango kikubwa, wanabebwa na mabao ambayo kwa bahati wamekuwa wakifunga, kikosi changu mimi ni bora, wachezaji wangu wana nguvu za kutosha na uwezo zaidi kuhakikisha tunashinda,” alisema.


Yanga tayari imewasili Bukoba kwa ajili ya mechi yao dhidi ya Kagera Sugar itakayochezwa kesho kwenye Uwanja wa Kaitaba

Mtete Focus Blog

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni