.

Jumatatu, 30 Septemba 2013

ZITTO ALAANI HATUA SERIKALI YA KUYAFUNGIA MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA...!!

Imeandikwa na Zitto Kabwe, Mb — Kwa mshtuko na masikitiko makubwa kuanzia jana jioni tumepokea taarifa za kufungiwa kwa magazeti mawili ya kila siku hapa nchini ya Mwananchi na Mtanzania. Serikali imechukua uamuzi huo kwa kutumia sheria ya kidikteta ya magazeti ya mwaka 1976 ambayo Tume ya Jaji Francis Nyalali iliiorodhesha kama sheria kandamizi. Sababu zilizotolewa kuhalalisha uamuzi huu ni sababu zisizo na maana na ambazo Serikali ingeweza kufungua mashtaka ya kawaida kabisa mahakamani kushtaki magazeti hayo iwapo haikupendezwa na habari walizochapisha.

Moja ya sababu ya kufungiwa kwa gazeti la Mwananchi ni kuchapisha taarifa kuhusu mishahara ya Serikali. Serikali inasema habari hii ni siri. Serikali hii hii ambayo imesaini makubaliano ya kuendesha serikali kwa uwazi (Open Government Initiative) na kumwagiwa sifa na Rais Barack Obama wa Marekani inalifungia gazeti kwa kuandika habari za mishahara ya watumishi wa Serikali. Mishahara kuanzia mshahara wa Rais mpaka wa mtendaji wa Kijiji haipaswi kuwa jambo la siri. Kuonyesha kuwa
jambo hili linapaswa kuwa wazi mkutano ujao wa Bunge tutatafuta kila namna kutaja mshahara wa Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na baadhi ya Watendaji wa Mashirika makubwa ya Umma kama njia ya kuwaunga mkono gazeti la Mwananchi kwa habari yao hiyo. Mapato ya Mbunge yanajulikana sasa kuwa ni shilingi milioni 11.2 kwa mwezi kabla ya kuongeza posho za vikao za shilingi laki 200,000 kwa siku na posho ya kujikimu ya shilingi 130,000 kwa siku. Watanzania wana haki ya kujua wanawalipa kiasi gani watumishi wao. Tutaanza na mshahara wa Rais!

Gazeti la Mtanzania limefungiwa pamoja na mambo mengine kwa kuandika 'mapinduzi ni lazima'. Inashangaza Serikali ya Chama cha Mapinduzi inaogopa neno mapinduzi. Marehemu Mzee Steven Salum Nandonde, aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Tandahimba alipata kusema bungeni kuwa 'lazima nchi ipinduliwe'. Ni matumizi ya lugha tu. Mzee Nandonde yeye alikuwa analalamikia maendeleo duni ya mikoa ya kusini na kutaka Kaskazini iwe Kusini na Kusini iwe Kaskazini. Serikali inafungia gazeti kwa sababu ya kuandika Mapinduzi ni lazima ilhali kila siku Zanzibar wanasema Mapinduzi daima!

Gazeti la Mtanzania linahaririwa na Absalom Kibanda, mwandishi wa habari ambaye bado anaponya majeraha ya mwili na kisaikolojia ya kuteswa na watu ambao mpaka leo hawajakamatwa. Badala ya Serikali kuwakamata watesaji wa Kibanda, inamnyima kazi Kibanda ili ateseke kwa njaa kwa kukaa miezi mitatu bila kazi. Pia wanatutesa Watanzania kwa njaa ya kupata habari ambayo ni haki ya msingi ya kikatiba. Hii ndio zawadi Serikali inampa Kibanda baada ya kung'olewa kucha, kunyofolewa jicho, kukatwa vidole na kuteswa kwa namna isiyoelezeka.

Matukio ya hivi karibuni na namna Serikali inavyoyachukulia yanaonyesha dhahiri kwamba Rais Kikwete kazidiwa nguvu na kundi la wahafidhina ndani ya chama na Serikali yake. Rais ambaye alianza kwa kuhubiri uvumilivu wa hali ya juu na hata yeye mwenyewe kupata kusema uvumilivu huu wengine wanauona kama udhaifu lakini ameamua kujenga Taifa la kuvumiliana. Rais alipata kulalamika hadharani kwamba kuna wenzake wanataka aongeze ukali. Ni dhahiri kundi hili la wahafidhina sasa ndio linalomwongoza Rais Jakaya Kikwete. Kitu kimoja tu Rais azingatie, kundi hili linaongozwa na maslahi binafsi ya kubakia kwenye utawala wakati yeye anapaswa kuacha 'legacy'. Rais Kikwete asipokuwa makini atakuwa Rais karatasi (lame duck) tu tunapoelekea mwisho wa utawala wake. Maamuzi ya hovyo na ya kidikteta ya kufungia magazeti yanamchora vibaya mbele ya wananchi na jamii ya kimataifa. Wahafidhina kuwa nguvu zaidi ya kiutawala ni makosa ambayo watanzania hawapaswi kuyakubali kamwe.

Wananchi sasa waifanye Serikali kujutia uamuzi wake wa kufungia magazeti. Nimeamua mimi binafsi kama mbunge kesho Jumatatu tarehe 30 Septemba, 2013 kupeleka taarifa rasmi kwa Katibu wa Bunge ya kupeleka muswada Bungeni wa kuifuta kabisa Sheria kandamizi ya magazeti ya mwaka 1976. Sasa tupambane na kundi dogo la wahafidhina ndani ya Serikali na CCM wasiopenda mabadiliko na iwe fundisho kwa wahafidhina wengine wowote waliopo ndani ya Serikali au nje ya Serikali kwamba Uhuru wa habari sio jambo la kuchezea kama gololi.

Mkenya aliyedaiwa kumteka Dk Ulimbokwa atozwa faini 1,000/- na kisha KUACHIWA HURU

TANZANIA YAONYWA KUHUSU KULEGA LEGA MCHAKATO WA EAST AFRICAN COMMUNITY

SEREKALI YA KENYA YAISHANGAA MAREKANI KWA KUSHAURI RAIA WAKE WASIENDE KENYA

UJENZI WA BARABARA ZA JUU (FLYOVERS) KUANZA 2014

MWANAMKE AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MITANO JELA BAADA YA KUMTUPA MTOTO WAKE CHOONI


Mwanamke mmoja mkazi wa Manga A Jijini Mbeya amehukumiwa kifungo cha miaka 5 jela kwa kosa la kutupa mtoto wake chooni. Mwaka huu katika eneo hilo baada ya watoto waliokuwa wakicheza kugundua kuwepo kwa Mtoto katika choo cha shimo.

Mtuhumiwa baada ya kukamatwa amekiri kutenda kosa hilo na kwamba alifanya hivyo baada ya mzazi mwenzie kumkataa.

Tumeona Mara Kwa Mara Dada Zetu Wakibadilisha Nywele Kumuiga Rihanna, Sijui Watafanya Ni Hii

BET Hip Hop Awards Cypher Mwaka Huu, Watakao Chana Ndio Hawa

Soma alichosema Solo Thang baada ya kufariki msanii Mack Malik na sikiliza hapa ngoma yao ya zamani “Ndani ya Party”

Msanii Mack Malik ambaye ni mmoja wa wasanii wanaounda kundi la Wateule, amefariki dunia. Mack Malik zaidi ya kuwa producer, pia alikuwa ni rapper. Solothang ameonyesha masikitiko yake kwa kumpoteza Mack Malik, soma maneno aliyoyaandika na sikiliza hapa ngoma yao ya zamani sana akiwa na Solothang. Ngoma hii ni moja kati ya ngoma kali za Solothang na chorus alisimama marehemu Mack Malik

New video : Navy kenzo ft A Pass – We do work

KIJANA ANASWA NA SHEHENA YA BANGI HUKO BUGURUNI..!!

Polisi wakikagua mahali alipokuwa amejificha mtuhumiwa wa bangi.

Msanii wa Bongo Fleva Amefariki Dunia, Malik Ahmed Maarufu Kama Mack Malik Simba Aka Mack 2 B Wa Wateule .


VIDEO: POLISI WATUMIA NGUVU KUWATAWANYA WANANCHI WALIOKUWA WAKIIBA MAFUTA BAADA YA LORI KUPINDUKA....

NJEMBA ACHEZEA KICHAPO CHA MACHANGUDOA BAADA YA KUGOMA KULIPA....!!


WAKATI Oparesheni Fichua Maovu (OFM) inayoendeshwa na Global Publishers ikiwa mzigoni, imenasa tukio la fedheha kwa njemba mmoja akichezea kichapo ‘hevi’ kutoka kwa wanawake waliosadikiwa kuwa machangudoa.
Katika tukio hilo lililojiri hivi karibuni majira ya asubuhi, maeneo ya Afrika Sana jijini Dar, jamaa huyo alidaiwa kuopoa changu ambaye alikwenda kumpa ‘mambo’ ya kiutu uzima kisha wakazinguana.
Mashuhuda wa tukio hilo ambao kwa sehemu kubwa walikuwa ni madada poa, walidai kuwa baada ya jamaa huyo kupewa huduma ya penzi jirani na eneo hilo aligoma kulipa hivyo timbwili zito likaibuka.

UKATILI!! MAMA AMNG'ATA BINTI YAKE SEHEMU ZA SIRI KWA KOSA LA KUJISAIDIA HAJA KUBWA OVYO....


MKAZI wa Kijiji cha Mlongazila, wilayani Kisarawe, Pwani, Moshi Hamad anatuhumiwa kumng’ata mwanaye, Khadija Hamad (6) sehemu za siri kwa madai ya kujisaidia haja kubwa na ndogo hovyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Tanzania Daima juzi wilayani Kisarawe, wakazi hao walisema mama huyo amekuwa na tabia ya kumfungia ndani mtoto wake huyo na kumchapa kwa zaidi ya nusu saa, akitumia nyaya za simu na kumng’ata sehemu mbalimbali za mwili zikiwamo za siri na kumsababishia maumivu makali.

Wakazi hao walisema waliamua kutoa taarifa kwenye dawati la haki za binadamu baada ya kuchoshwa na vitendo hivyo, na sasa wamelitaka Jeshi la Polisi kumkamata mama huyo na kumchukulia hatua.

Stella Musa, alisema sehemu za siri za mtoto huyo zimeharibiwa kutokana na kung’atwa na meno, huku zikiwa na vidonda vinavyodaiwa vimetokana na kuchomwa na kitu chenye ncha kali.

“Wazazi wa mtoto huyo ni wanangu, siku moja mama huyo alimuumiza mkono. Nilimchukua na kukaa naye nyumbani kwangu kwa mwezi mmoja nikimuhudumia kwa kumkanda kwa maji ya moto,” alisema Stella.

Mwalimu wa Shule ya Msingi Mlongazila, Paulo Idana ambaye pia ni katibu wa dawati la kutetea haki za binadamu, alisema suala hilo limewafikia, hivyo wanachukua hatua za kisheria huku mtoto huyo amewekwa chini yao kwa matibabu zaidi.

“Tulimfuata mama huyo Septemba 20 mwaka huu na tulifanya nae mahojiano mbele ya ofisa mtendaji wa kijiji na alikiri akisema alifanya hivyo kwa sababu ya hasira. Tunafanya utaratibu ili tumfikishe kwenye vyombo vya sheria,” alisema Idana.

Akieleza mkasa huo, mtoto huyo alisema wakati mwingine mama yake alikuwa akimwita ili amfundishe kusoma na aliposhindwa aling’atwa mgongoni, mapajani na sehemu za siri huku akisema atamfanyia hivyo hadi ajue kusoma.

Mama wa mtoto huyo, Moshi, alisema alikuwa akitoa adhabu kwa mwanaye huyo kutokana na kujisaidia haja ndogo na kubwa hovyo wakati akirudi shule.

“Nafanya hivi kutokana na hasira siwezi nikamuona mtoto wangu anajisaidia haja kubwa na ndogo kwenye nguo nikamwacha tu, lazima nimwadhibu… jana alitapika kwenye sahani. Je, mtoto kama huyu nitamwacha?” alihoji Moshi.

Mwenyekiti wa kitongoji hicho, Khadija Samizi alikiri kuwepo kwa tukio hilo.

-Tanzania Daima

SERIKALI YASUTWA KWA KUYAFUNGIA MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA....YADAIWA KIKWETE KAZIDIWA NGUVU.....

Jumapili, 29 Septemba 2013

Rapper Wako Bora Nikki Mbishi Kutoka Tamaduni Musik Ametoa Cover La Album Yake Mpya, Liko Hapa



RIPOTI KAMILI YA KIFO CHA DADA WA MWEKITI WA CHADEMA MH. FREEMAN MBOWE ALIYEPINDUKA NA GARI...!!!


DADA wa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amefariki papo hapo baada ya gari alilokuwa akiendesha kupasuka tairi ya mbele na kuingia chini ya daraja baada ya kupinduka na kusababisha watu wawili kufa na wengine watatu kujeruhiwa vibaya.

Dada huyo, Grace Aikaeli Mbowe, anayesadikiwa kuwa na umri kati ya miaka 47 hadi 50, alikuwa akiendesha gari yenye namba T 277 CAJ aina ya Toyota Cresta akiwa na mumewe aliyefahamika kwa jina la Ibrahim Lukindo (52), wakitokea Jijini Tanga, walipata ajali hiyo eneo la Kabuku wilayani Handeni.

Kamanda wa polisi mkoani Tanga (ACP) Costatine Massawe alisema kupitia Ofisa wake wa upelelezi mkoani Tanga, Bw Aziz Kimata, kwamba ajali hiyo ilitokea majira ya saa 1:30 asubuhi jana katika eneo hilo baada ya gari hilo kupasuka tairi ya mbele kulia na kisha kuingia chini ya daraja lililokuwepo eneo hilo.

"Ni kweli kuna ajali ilitokea eneo la Kabuku gari aina ya Cresta lililokuwa likiendeshwa na ndugu inavyosemekana wa Bw Freeman Mbowe, limepata ajali baada ya kupasuka tairi la mbele na kuacha barabara na kuingia chini ya daraja .

"Dereva anayeitwa Grace Aikael Mbowe na mtu anayesemekana ni mumewe anayeitwa Ibrahim Lukindo, wamefariki na watu watatu waliowachukua wamejeruhiwa," alisema RCO Kimata.

Aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni pamoja na Bw Ridhiwani Bakari (29) aliyekuwa na mkewe Zeddy Nzuke (29) raia wa Kenya aliyekuwa na mtoto wake mwenye umri wa miaka miwili na miezi minne aliyefahamika kwa jina la Mariam Ridhiwan ambao kwa sasa wamelazwa katika hospitali ya Magunga wilayani Korogwe.

RCO Kimata aliyezungumza kwa niaba ya kamanda huyo wa polisi alisema chanzo cha ajali hiyo inasemekana kimetokana na kupasuka kwa mpira huo na mwendo kasi wa kawaida na kwamba majeruhi na maiti zi9mehifadhiwa kwenye hospitali hiyo.

Mwandishi wa habari hizi, aliyefika kwenye hospitali hiyo na kuzungumza na Ridhiwani pamja na mkewe ambaye amelazwa wodi namba mbili ya wanawake katika hospitali hiyo, alisema kwamba ndoto zake za kufanya kazi Dar es salaam zimezimika ghafla kutokana na kwamba alikuwa aende kupamba kazi ya uofisa ugavi katika taasisi moja ya fedha ya marehemu Mbowe Jijini Dar es salaam.

"Nilikuwa naenda kupewa kazi na mama Mbowe katika Institution yake ya Micro-Financial Jijini Dar es salaam, mimi ni procurement (Mgavi-manunuzi) na ni Mkenya kwetu ni Eastern Province Kang'undo na nimeolewa na bwana Mtizedi...Lakini sasa ndoto zangu za kufanya kazi Dar es salaam zimezimika ghafla," alisema Zeddy akiwa kitandani amelala na mwanwe ambaye alikuwa haongei tangu amefika katika hospitalini hapo.

Mumewe na mwanamke huyo akizungumzia ajali hiyo alisema kuwa hakuwa akijua kwani alikuwa amelala dakika tatu kabla ya kutokea ajali hiyo ambapo alishtukia yeye, mkewe na mwanawe wametupwa chini kwenye majani wakiwa hawajijui na walikimbizwa katika hospitali hiyo ya Korogwe

Ridhin ambaye ni mkazi wa Nguvumali Jijini Tanga, alisema safari yao hiyo ilikuwa ifanyike Jumamosi mchana lakini kutokana na na kuchelewa kwa wenyeji wao hao, waliondoka Tanga kwenye hoteli ya Doliphin walikolala majira ya saa 11:00 alifajiri kwa ajili ya kwenda Jijini Dar es salaam.

Muuguzi wa zamu wa hospitali hiyo Bi Nayela Missingo alikiri kuwapokea wagonjwa hao ambapo alisema wanafanya jitihada za kuwahamishia katika hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam mtoto Mariam ambaye amepata majeraha katika kichwa chake na kwamba tangu afikishe hospilaini hapo hakuwa katika hali nzuri, haongei walakunyonya.

Magazeti ya leo Jumatatu September 30 2013 na Habari za Udaku, Michezo na Hardnews