.

Alhamisi, 17 Oktoba 2013

Huyu ndio mmoja kati ya wasanii wanne wa nje watakaodondoka kwenye Fiesta 2013

Clouds Media leo hii wamethibitisha kuwaleta wasanii zaidi ya watatu kutoka nje ya Tanzania (International artist), na leo hii wamethibitisha kudondoka kwa msanii kutoka
Nigeria Davido anaefanya poa sana Africa na single kadhaa kali, ikiwemo Gobe.
Davido akiongea  kutangaza ujio wake
Wasanii zaidi ya 40 kutoka Tanzania watapanda jukwaa hilo la Fiesta na leo hii imetoka list ya wachache tu wakiambatana na Davido ambao ni Afande Sele, Makomando, Mr Blue, Young Killer,  Young D, G Nako, Joe Makini, Nikki wa pili, Kala Jeremiah na Chidi Benz, list itaendelea siku ya kesho ambapo utamsikia msanii mwingine wa nje atakae tua bongo pamoja na muendelezo wa list ya wasanii wa hapa hapa.
Fiesta itarajiwa kufanyika siku ya jumamosi ya tarehe 26 ndani ya viwanja vya leaders.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni