.

Ijumaa, 11 Oktoba 2013

KUHONGWA KWA LINAH KWAIBUA MAMBO....SOMA ZAIDI HAPA

MAELEZO ya hivi karibuni aliyodaiwa kuyatoa mwanamuziki Estelina Sanga ‘Linah’ mtandaoni kuwa mtaji wake katika kazi za ujasiriamali ameupata kwa kuhongwa na mpenzi wake na kuchanganya na pesa zake yameibua mambo.
 
 
Wakionesha kushangazwa kwao na maelezo hayo, baadhi ya mashabiki wake walisema kitendo cha yeye kukiri kuwa anahongwa kinawashawishi wasichana wengine wahisi nao bila kuhongwa hawawezi kufanikiwa.

“Huyu anasema mtaji wake ameupata kwa kuhongwa na mpenzi wake, ina maana asingehongwa asingefika hapo alipo? Na sisi tutafute wa kutuhonga ili tufanikiwe? Lakini kwani mpenzi wako akikupa pesa anakuhonga? Linah asitupotoshe,” alisema Neema Kiza.


Mdau mwingine ambaye hakupenda kutaja jina lake alisema: “Eti anasema amehongwa na mpenzi wake, sasa anatuambia ili iweje? Hata hivyo, mpenzi wako anapokupa pesa hakuhongi, anakusaidia, alijue hilo.”
 
Mtete Focus Blog.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni