.

Jumamosi, 28 Desemba 2013

Mambo 10 ya kufahamu kuhusu huyu Msomali alieigiza kwenye Captain Phillips.


Msomali 1Ni movie ambayo nimeitazama Cinema wiki kadhaa zilizopita, stori ya ukweli jinsi meli ya mizigo ilivyotekwa na Wasomali ambao kazi yao ni kushinda baharini kutekeleza maagizo ya Boss wao, kuteka meli za kigeni na kudai malipo makubwa ya pesa.
Yafuatayo ni mambo kuhusu Mwigizaji Barkhad Abdi ambae amecheza kama kiongozi wa watekaji hao wa Kisomali kwenye hii movie ambayo kila wakati inakupa hamu utake kujua nini kinafata.
1. Alikua anapenda kuigiza movie lakini hakuwahi kufanya hivyo kabla, hii ya Captain Phillips ndio ya kwanza.
2. Kwa kipindi kirefu amekua nyuma ya Camera tu akishoot music videos lakini hakuwahi kuwa mbele ya Camera.
3. Ni raia wa Somalia ambae kwa miaka kadhaa sasa amekua akiishi nchini Marekani na alipata dili la kuigiza hii movie kwa kujitokeza baada ya kuona ikitangazwa kwenye TV kwamba anatafutwa mwigizaji wa Kisomali.
tom hanks 24. Wakati wanaanza kuigiza ile scene ya kwenye kuteka meli ndio siku yake ya kwanza alimuona live Starring Tom Hanks, walikua hawajawahi kuonana kabla.
5. Kabla ya kuanza kuigiza movie, Barkhad alipewa mafunzo makubwa ya vitu ambavyo alikua havijui mfano kuogelea, kutumia silaha, kupanda na kupigana… vyote alikua havijui kabisa ambapo baada ya mafunzo yeye na wenzake walikua na hamu ya kukutana na Tom kwa mara ya kwanza lakini Director alikataa na kusema watamuona kwenye siku ya kwanza ya kuanza kuigiza movie.
Msomali 36. Kabla ya kujitokeza kuwania nafasi ya kuigiza kwenye hii movie kuna Wasomali wenzake walimfata na kumwambia kuigiza kwake kwenye hii stori hakutawapendeza watu wa Somalia ila yeye anasema hakuichulia kwenye njia hiyo na anaamini wataelewa.
7. Kwa sasa Abdi anaishi Minneapolis nchini Marekani.

8. Anasema bado ana ndugu zake wengi wanaishi Somalia na wengine hata hajawahi kuwaona maishani, wengine toka alivyoondoka nchini humo akiwa na umri wa miaka saba.
9. Anaamini siku moja atarudi nchini mwao hata kusalimia.
10. Kwa sasa mpango mkubwa wa Abdi ni kutaka kuigiza zaidi.
msomali 2



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni