.

Jumanne, 19 Novemba 2013

MSANII WA VICHEKESHO WA BONGO BAADA YA KUDATE NA MADEMU ZAIDI YA 500, SASA AMUA KUWEKA WAZI MAJIBU YAKE YA VIPIMO VYA UKIMWI:



Ama kweli acheni mungu aitwe Mungu Msanii aliyeshika ustaa namba moja Tanzania kwa skendo za picha za utupu Manaiki Sanga " The Don" amepima gonjwa hatari la UKIMWI na vipimo vimeosha hana kabisa dalili zozote za ugonjwa huo huku wanawake kadhaa wakifanya sherehe kwa tukio hilo.

 PAPARAZI ambayo imenasa cheti cha Manaiki ambacho kinaonesha alipima tarehe 13/9/2013 kwenye Hosptali ya
Magomeni huku akishuhudiwa na jamaa na marafiki.
Hata hivyo katika hatua nyingine inadaiwa kuna staa mmoja ndiye aliyemlazimisha Manaiki kwenda kupima UKIMWI ka makubaliano kama ataonekana mzima basi atampa penzi hivyo ilimlazimu Manaiki kufanya hivyo bila hiyana.

Taarifa za Manaiki kugundulika hana Ngoma zilianza kusambaa mji mzima baada ya kuvuja hali iliyowafanya mabinti mbalimbali walipitiwa na msanii huyo kufanya sherehe " Unaambiwa bmara baada ya taarifa kuvuja kuwa Manaiki hana Ukiwmi wasichana walifurahi sana huku wengine wakiangua vilio kwa furaha kutokana na uvumi wa awali kuwa huenda Manaiki alikuwa sio mzima ndioa maana aliamua kutembea na wanawake wote hao.  
 Manaiki hadi sasa anaendelea kushikiria vichwa vya habari kwenye mitandao ya kijamii na magazaeti pendwa kwa kashfa ya kutembea na wanawake zaidi ya mia nane bila kinga na kupiga nao picha za utupu kisha kusambazwa mitandaoni.

PAPARAZI ilimtafuta Manaiki Sanga kupitia simu yake ya mkono na kwa bahati nzuri alipatikana na kutoa kauri " Ndiyo nimepima kwa hiari yangu si unajua kujua afya yako ni kitu cha msingi katika maisha hivyo haikuwa shindikizo la mtu mimi mwenyewe niliamua tu kufanya hivyo" Alisema Manaiki ambae yuko Jijini Arusha kimaigizo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni