.

Ijumaa, 27 Septemba 2013

Msimu Kwa Mara Ya Kwanza Bila Mzee Alex Ferguson, Fuatilia Hapa


Manchester United imetoa picha yao ya kikosi kwa msimu mpya akiwemo meneja mpya David Moyes, Marouane Fellaini na Wilfried Zaha wakiwa ni ingizo jipya kikosini
Wakati Manchester United ikitoa picha yao ya kwanza maalum bila ya Sir Alef Furguson, mstari wa mbele umebadilika kwa mara ya kwanza tangu miaka 27 iliyopita ambapo David Moyes ametokezea katika sehemu ya kati katika picha hiyo tangu kujiuzulu kwa Sir Alex Ferguson. Picha hiyo imeachiliwa kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter, ambapo Moyes akiwa kati ya Nemanja Vidic na kiungo mkongwe Ryan Giggs. Picha hiyo pia inamuonyesha nyota mpya Marouane Fellaini, ambaye yuko mstari wa nyuma katikati na Wayne Rooney, ambaye alihusishwa na kutaka kuihama klabu hiyo majira ya kiangazi.
Katika picha hiyo pia Giggs na Vidic wanaonekana wakiwa wameshikilia taji la ligi kuu "Premier League" ngao ya Jamii "Community Shield".

KIKOSI CHA MSIMU CHA MANCHESTER UNITED 2013-2014
The Manchester United squad (Back Row L-R:) Danny Welbeck, Phil Jones, Chris Smalling, Jonny Evans, Marouane Fellaini, Rio Ferdinand, Michael Carrick, Robin van Persie (Third Row L-R:) Masseur Garry Armer, Performance Analyst Paul Brand, Head of Fitness Tony Strudwick, Antonio Valencia, Darren Fletcher, Wilfried Zaha, Adnan Januzaj, Fabio da Silva, Masseur Rod Thornley, Kit Manager Alec Wylie, Physio Neil Hough (Second Row L-R:) Assistant Kit Manager Ian Buckingham, Physio Rob Swire, Dr Steve McNally, Alexander Buttner, Sam Johnstone, Anders Lindegaard, David de Gea, Ben Amos, Ashley Young, Coach Phil Neville, Masseur Andy Caveney, Goalkeeping Coach Chris Woods. (Front Row L-R:) Shinji Kagawa, Rafael da Silva, Anderson, Nani, Assistant Manager Steve Round, Ryan Giggs, Manager David Moyes, Nemanja Vidic, Coach Jimmy Lumsden, Patrice Evra, Javier "Chicharito" Hernandez, Tom Cleverley and Wayne Rooney

Katika picha hiyo hawaonekani wasaidizi wa Furguson Mike Phelan, Rene Meulensteen na Eric Steele ambao nafasi zao zimechukuliwa na Steve Round, Jimmy Lumsden na Chris Woods.

Paul Scholes, ambaye huko nyuma alikuwa karibu na Ferguson, hatakuwa na pichani baada ya kustaafu baadaye huku Nick Powell na Federico Macheda hawakuwepo katika picha hiyo kwakuwa wako kwa mkopo katika vilabu vingine.

Vijana Wilfried Zaha na Adnan Januzaj pia wako pichani huku Phil Neville akirejea kama kocha..

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni