.

Alhamisi, 25 Septemba 2014

Wafuasi wa Boko Haram wajisalimisha


Wanamgambo wa Boko Haram
Jeshi la nchini Nigeria limesema zaidi ya wafuasi 260 wa Boko Haram wamejisalimisha kaskazini mwa nchi hiyo.
Jeshi hilo limesema katika mapambano limemuua mtu mmoja ambaye huwa anaonekana kwenye picha za video za propaganda za Boko haram wakishuku kuwa huenda ni Kiongozi wa wa kundi hilo, Abubakar Shekau.
Mwandishi wa BBC nchini Nigeria amesema kuwa majuma ya hivi karibuni Boko Haram imeshindwa kwa kiasi kikubwa wakati walipokuwa wakipambana kudhibiti eneo karibu na mji wa Maiduguri.
Jeshi limesema wafuasi 135 wa Boko Haram wamejisalimisha wakiwa na silaha zao katika majimbo ya Biu na Borno,halikadhalika wafuasi wengine 133 wanahojiwa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni