.

Alhamisi, 11 Septemba 2014

10 PICHAZ: AJALI YA BASI LA RUKSA YAUA WAWILI NA KUJERUHI 65 KIGOMA!

Basi la Ruksa aina ya Scania lenye namba za usajili T 273 ACX llililokuwa ikitokea mkoani Kigoma kwenda wilayani Kahama mkoani Shinyang'a likiwa limepata ajali katika kijiji cha Kanyonza wilayani Kakonko,mkoani Kigoma ambapo watu Wawili walipoteza maisha papo hapo na wengine 65 kujeruhiwa katika Ajali hiyo ya Septemba 08,2014,majira ya saa Sita mchana.
Pichani juu na chini ni Jeshi la polisi wilaya ya Kakonko lilifika eneo hilo na kuwachukuwa waliojeruhiwa  na kuwapeleka katika hospitali ya wilaya  kwa ajili ya matibabu.
 Pichani ni Baadhi ya Majeruhi wa ajali hiyo wakiwa wodini  katika hospitali ya wilaya ya Kakonko kwa ajili ya matibabu.
 Taswira ya Basi hilo la Ruksa likiwa eneo la Ajali ambapo mashuhuda wanasema chanzo cha ajali kilisababishwa na mwendo kasi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni