.

Ijumaa, 25 Julai 2014

Lulu Michael Amfungukia Ali Kiba

Ali Kiba ameachia  nyibo mbili  kwa  mpigo ambapo response ya mashabiki ni nzuri. Sasa kupitia Instagram star wa filamu nchini Elizabeth Michael ‘Lulu” amefunguka mambo mengi  sana  kuhusiana  na  Ali Kiba…….Hiki  ndicho  alichokisema:
 
“Haya sasa…..maelezo hatimaye yamepatikana….mnivumilie ni marefu Kidogo…! 
 
1. Pongezi kwa @officialalikiba nimesikia Mwana wa Dar es Salaam tu lkn kiukweli Mimi binafsi umenikonga moyo…! 
 
2. Ieleweke kwamba Mimi ni shabiki wa mziki mzuri hata ukiwa umeibwa na underground na wengi wenu mmekuwa mashaidi maana huwa na post video nikiimba miziki ya watu tofauti hata wasio mastar wakubwa…kwahyo mm sio shabiki wa mtu ni shabiki wa kazi ya mtu
Elizabeth Michael ‘Lulu’
Elizabeth Michael ‘Lulu’


 3.Nimegundua wasanii wengi wa Tanzania tuna U mimi….hivi ulaya wangekuwa hvyo…Hollywood c kungekuwa na mtu mmoja tu au wawili basi….nadhani umefika muda wa wasanii Kama wasanii kila mmoja kujiamini ktk kazi Zake na kufikiria kufanya makubwa sio kufikiria kushindana na flani…..tena tukishirikiana tutaweza kufika mbali zaidi ya hapa…tutaendelea kila cku kuona maajabu wenzetu Nigeria wanafika mbali….wanajielewa na wanashirikiana…!Kama binadamu kukoseana kupo ila ukijua kosa kuomba msamaha na kuendelea na maisha ndo busara zaidi

 4.Hapa sasa….nieleweke jmn…Mashabiki wetu Tunawapenda sawa….lakini kwa namna moja au nyingine Mashabiki mnchangia bifu za wasanii….JAMANI Ukiwa shabiki wa Lulu haimaanishi umchukie Wolper(mfano)Kama ww ni shabiki wa mtu sio umchukie msanii mwingine na hii kwakweli ninaiona Tanzania tu(thou sio Mashabiki WOTE) 

5. Mwisho…WOTE tunategemeana wasanii tupendane tukiona wenzetu flani wana shida tusaidie kuondoa tofauti na Mashabiki pia nyie ndo msaidie kupatanisha watu sio kuchochea ugomvi….
 
Mungu alivyotuumba wengi alikuwa na maana yake sasa we ukitaka uwe Mkali pekeyako ungeumbwa mwenyewe ukawekwa kwenye dunia ya pekeyako tukusome kwenye history dunia flani Kuna mtu mkali yuko pekeyake..!duh nimechoka kuandika lkn cjamaliza…..bt I real wish wakali mngeungana mfanye mambo makubwa….naamini inawezekana…!”

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni