Mfano kuvaa nguo ya aina moja hiyohiyo kila wakati, wengine huwa wanatembelea magari mabovu kabisa lakini watoto wao na wake zao wanatembelea magari makali na wanabadilisha kila wakati, wengine tunaambiwa wanalala barazani.
Sasa hii ya tajiri wa mtandao wa kijamii wa Facebook wenye watumiaji zaidi ya bilioni moja kote duniani Mark Zuckerbeg sijui watu wataiweka kwenye kipande gani manake ameonekana mara nyingi sehemu na nyakati tofauti akiwa amevaa Tshirt moja tu ya kijivu.
‘Nimepata hii bahati ya kipekee kuwa kwenye nafasi niliyonayo, ninaamka kila siku na kuwahudumia zaidi ya watu bilioni moja duniani… naona sitofanya kazi yangu vizuri kama nitatumia muda wangu kwenda kutafuta/kuchagua nguo nzuri, tshirt mnayoniona nayo ni ya rangi moja lakini nilizinunua nyingi za namna hii’
‘Ni Tshirt ambayo sio moja… ninazo nyingi ila zinafanana, muda wangu mwingi nimeutenga kwa ajili ya kuhudumia watu na sio kujihudumia mimi kwenye kuchagua nguo nzuri, mavazi ni kitu kidogo sana kwangu’
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni