.

Jumatano, 27 Agosti 2014

Baada ya kutemwa na Bosi wake BABY MADAHA Ajipumzisha kwa Msanii WYRE



MWANADADA  anayefanya vizuri katika muziki Bongo, Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’ kwa sasa amejiweka kimapenzi na msanii anayetamba Kenya, Kevin Wyre baada ya kuwepo kwa tetesi za kutemana na mtu wake wa awali, Joe Kairuki aliyekuwa pia ni meneja wake.
WYRE
Watu walio karibu na wawili hao wanasema uhusiano huo unafanywa kwa siri ili usivuje na kwamba kwa  sasa pia wanafanya kazi ya pamoja itakayokuwa hewani wakati wowote muda mfupi ujao.

Alipoulizwa juu ya ishu hiyo, Baby Madaha alitiririka: “Mimi nina uhuru wa kufanya chochote ninachojisikia na hakuna mtu atakayeweza kuniingilia katika maisha yangu wala uhusiano wangu kwa sababu sigongi kwa mtu kuomba msaada.”

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni