.

Alhamisi, 2 Oktoba 2014

KIBONDE GADNER WAPANDISHWA KIZIMBANI LEO


Kibonde na Gadner wakiingia kwenye Mahakama ya Kinondoni leo.
Gadner akielekea chumba cha mahakama.Gadner na Kibonde wakitoka eneo hilo la mahakama.

SAKATA la kesi ya watangazaji wawili, Ephrahim Kibonde wa Clouds FM na Gadner G. Habash wa Times Fm wanaokabiliwa na kesi ya kugonga na kusababisha uharibifu wa gari na kisha kutotii amri ya askari wa usalama barabarani baada ya kufanya kosa hilo katika eneo la Makumbusho jijini Dar es Salaam, Agosti 9 mwaka huu, wamefikishwa tena katika Mahakama ya Kinondoni kujibu mashtaka yanayowakabili.
Wakisomewa mashtaka hayo na mwendesha mashtaka wa serikali, Ramadhan Mkimbu mbele ya Hakimu Mkazi, Aniceta Wambura alisema washtakiwa walitenda makosa hayo huku wakijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.
Mshtakiwa wa Kwanza, Eprahim Kibonde anakabiliwa na makosa mawili ambapo kosa la kwanza ni kuendesha gari huku akiwa amelewa, kosa la pili ni kugonga gari na baada ya kufanya kosa hilo alikataa kutiii amri ya Sajent Silvester wakati huo huo, Gadner anakabiliwa na kosa la kutotii amri na kutoa lugha ya maneno mbele ya askari.
Kesi hiyo imesogezwa mbele hadi Novemba 5 na 21 itakapoanza kutolewa ushahidi baada ya washtakiwa wote kuiomba mahakama ifanye hivyo kutokana na mwanasheria anayesikiliza kesi yao kupatwa  na dharura.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni