Sasa taarifa mpya iliyotoka baada ya hii picha kuzidi kusambaa ni kwamba Jeshi la Polisi Kagera limechukua maamuzi ya kuwafukuza kazi askari hawa wawili pamoja na mwingine mmoja ambae ndio aliipiga hii picha kupitia simu yake ya mkononi.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Henry Mwaibambe amewataja askari hao kuwa ni PC Asuma Mpaji Mwasumbi mwenye namba F.7788,PC Fadhili Linga mwenye namba G 2122 na PC Veronica Nazaremo Mdeme na wote walikuwa askari wa kikosi cha usalama barabarani wilayani Missenyi.
Mwaibambe amekiri kuwa picha husika inayoonekana kwenye mitandao ni
picha halisi ambayo haijachakachuliwa hivyo ni wazi kila askari kujua
maadili ya kijeshi yapo kisheria na askari yeyote anafundishwa namna ya
kuishi katika maisha ya utumishi wa jeshi la Polisi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni