DRC-MONUSCO-HRW-Haki za binadamu -
Makala iliyochapishwa tarehe : Ijumaa 04 julai 2014 -
Taarifa za ivi karibuni : Ijumaa 04 julai 2014
Wanajeshi wa kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini Congo (Monusco) wakipambana dhidi ya makundi ya waasi..
REUTERS/Kenny Katombe
Shirika la kimataifa linalo tetea haki za binadamu lenye
makao yake makuu nchini Marekani la Human Right Watch limelituhumu jeshi
la jamhuri ya kidemokrasia ya Congo la FARDC pamoja na vikosi vya Umoja
wa Mataifa nchini humo Monusco kwa kupuuzia kuzuia kutokea kwa machafuko ya mwezi uliopita huko mashariki mwa DRCongo.
Shirika hilo limesema majeshi ya Congo na yale ya Monusco
hayakuingilia kati ili kukomesha machafuko yaliogharimu maisha ya watu
zaidi ya 30 na ambayo yalitokea katika kijiji cha Mutarule katika usiku
wa Juni 6 kuamkia Juni 7 katika mkoa wa Kivu ya KusiniHivi karibuni kiongozi wa majeshi ya Monusco nchini DRCongo Martin Koble alibaini maskitiko yake kuona vikosi vya Umoja wa Mataifa vilishindwa kuziia mauaji hayo yasitokei.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni