.

Jumatano, 5 Februari 2014

Kilichosemwa na Basata kuhusu kufungiwa kwa video kadhaa hapa Bongo ikiwemo ya Snura.


godSiku kadhaa zilizopita kupitia millardayo.com kuna taarifa ziliztoka kuhusu kufungiwa kwa video ya Nimevurugwa ya Snura,taaarifa hizi alizi-amplify meneja wake Snura ‘Hk’ akidai kuwa sababu maalum bado hawajazipata ingawa kila kituo anachoenda wanampa sababu tofauti.
Millardayo.com haikuishia hapo ilienda moja kwa moja kwenye Baraza la Sanaa la Taifa(Basata)ili kuujua undani wa sakata hili ikiwemo pia kuulizia video ya Jux(uzuri wako)ambayo nayo ilitoka taarifa ya kufungiwa kwa video hiyo.
Kutoka Basata huyu hapa Godfrey mungeleza ni kaimu katibu mtendaji  anataarifa zaidi>>Unaposema kufungia video moja kwa moja kuna chombo kingine cha serikali kinashughulikia hilo ambao ni bodi ya filamu Tanzania’
‘Bodi ya filamu wanaangalia video zote suala zima la filamu wanapoona hii haikidhi au haifai kwa jamii za Kitanzania basi wanaisimamisha kidogo wanamshauri aweze kuirekebisha ili iweze kulingana na maadili ya kitanzania’
‘Sisi tunaangalia Audio kabla haijaingia sokoni katika urasimishaji tunakaa tunausikiliza muziki wake tunashauriana kwamba akarekebishe hapa na tunaangalia mambo mengi ikiwemo ubunifu wake mwenyewe’
‘Suala la kufungiwa kwa Snura najua kabisa linaenda kwenye suala la maadili na limeandikwa sana na sisi Baraza kama Baraza tunaangalia sana suala la maadili tukisema tunamfungia hatufungii video tu tunamfungia msanii mwenyewe’

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni