.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo MAJANGA. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo MAJANGA. Onyesha machapisho yote

Jumanne, 14 Oktoba 2014

Ebola:Matamshi ya Chris Brown yakera


Mwimbaji Chris Brown
Mwimbaji mashuhuri duniani ,Chris Brown ametuma ujumbe kwenye mtandao wa Twitter Jumatatu kuhusu ugonjwa wa Ebola na kutoa maoni yake.
''Sijui , lakini nadhani Janga la Ebola ni njia moja ya kudhibiti idadi ya watu duniani...janga hili linatisha kweli,'' aliandika Brown.
Saa chache baadaye alionekana kufahamu uzito wa kauli yake na ambavyo uliwakera watu kwenye mtandao huo na baadaye kusema....''afadhali nikimye.
Ujumbe wa Brown ulisambazwa mara 16,000 kwenye mtandao wa Internet.
Hata hivyo watu hawahukufurahia matamshi ya Chris Brown kwani walaionekana wakimjibu kwa ukali baadhi wakisema, mwimbaji huyo anapaswa kunyamaza ikiwa hana cha kusema.
Janga la Ebola limesababisha vifo vya zaidi ya watu 4000 katika kanda fa Afrika Magharibi.
Ugonjwa huo umeenea hadi Uhispania na nchini Marekani ambako mgonjwa mmoja aliyueingia nchini humo akiwa ameambukizwa Ebola alifariki wiki jana.

Alhamisi, 11 Septemba 2014

10 PICHAZ: AJALI YA BASI LA RUKSA YAUA WAWILI NA KUJERUHI 65 KIGOMA!

Basi la Ruksa aina ya Scania lenye namba za usajili T 273 ACX llililokuwa ikitokea mkoani Kigoma kwenda wilayani Kahama mkoani Shinyang'a likiwa limepata ajali katika kijiji cha Kanyonza wilayani Kakonko,mkoani Kigoma ambapo watu Wawili walipoteza maisha papo hapo na wengine 65 kujeruhiwa katika Ajali hiyo ya Septemba 08,2014,majira ya saa Sita mchana.
Pichani juu na chini ni Jeshi la polisi wilaya ya Kakonko lilifika eneo hilo na kuwachukuwa waliojeruhiwa  na kuwapeleka katika hospitali ya wilaya  kwa ajili ya matibabu.
 Pichani ni Baadhi ya Majeruhi wa ajali hiyo wakiwa wodini  katika hospitali ya wilaya ya Kakonko kwa ajili ya matibabu.
 Taswira ya Basi hilo la Ruksa likiwa eneo la Ajali ambapo mashuhuda wanasema chanzo cha ajali kilisababishwa na mwendo kasi.

Ijumaa, 5 Septemba 2014

Ajali ya Mabasi Yaua Watu 36 na kujeruhi 76 mjini Musoma PICHA 50 HAPA


Basi la Kampuni ya J4 EXPRESS lenye nambari za usajili T 677 CYC lililokuwa likitoka Musoma kuelekea Kilari Mkoani Mara likiwa limeumia vibaya sana baada ya kugongana uso kwa uso na Basi lingine la Kampuni ya MWANZA COACH lenye nambari za usajili T 736 AWJ katika eneo la SabaSaba,Mjini Musoma leo  mchan.

Watu 36 wamepoteza maisha papo hapo na wengine kujeruhiwa vibaya sana.Kwa mujibu wa Ripota wetu aliyekuwa eneo la tukio,inaelezwa kuwa chanzo cha ajali hiyo ni  kuwa Basi la J4 ambalo lilikuwa likijaribu kuipita gari ndogo aina ya Nissan Terano lenye nambari za usajili T 332 AKK katika sehemu ambayo mbele kuna daraja linaloweza kupitisha gari moja kwa wakati huo,kutokana na kuwa basi hilo lilikuwa kwenye mwendo kasi liliweza kuisukuma kwa ubavuni gari hiyo ndogo ambayo haikuweza kuhimili nguvu ya Basi hilo na kutoka kwenye njia na kwenda kuingia mtoni, hali iliyoipelekea basi hiyo kuamini kuwa itawahi kupita katika daraja hilo bila kufahamu kuwa Basi lingine linalokuja mbele nalo liko kwenye mwendo kasi huku nalo likitaka kuwahi kupita kwenye daraja hilo.
ajali
Ndani ya gari hiyo ndogo kulikuwa na watu watatu,ambapo wawili wamefariki na mmoja amejeruhiwa.
Basi la Kampuni ya MWANZA COACH lililokuwa likitokea Musoma kwenda Mwanza linavyoonekana baada ya kugongana uso kwa uso na Basi la Kampuni ya J4 EXPRESS.
Umati wa Watu ukiwa umekusanyika kwenye eneo hilo ilikotokea ajali hiyo mbaya na kusababisha watu 36 kupoteza maisha wakishuhudia tukio hilo la ajali.


Guldoza likifanya kazi ya kuichomoa gari ndogo aina ya Nissan Terano lenye nambari za usajili T 332 AKK lililoshukumwa na basi hilo mpaka kuingia mtoni.Gari hii ilikuwa na watu watatu,ambapo wawili wamefariki dunia na mmoja kujeruhiwa.

Sehemu ya waokoaji waliofika kwenye tukio hilo.
Wanausalama wakijadiliana jambo kwenye eneo hilo la tukio.
 
Baadhi ya Mizigo ya abiria wa mabasi hayo wakiwepo waliopoteza maisha.
Uokozi ukiendelea.
Askari Polisi wakitoa miili ya watu wawili waliokuwemo kwenye gari hiyo.
Tupe maoni yako hapo Chini..!!

Jumatano, 3 Septemba 2014

Nyumba ya Big Brother yateketea A.Kusini


Cherise Makubale wa Zambia ndiye alikuwa mshindi wa kwanza wa Big Brother
Uzinduzi wa makala mapya ya kipindi maarufu cha Big Brother nchini Afrika Kusini umeahirishwa baada ya moto mkubwa kuteketeza studio za kipindi hicho mjini Johannesburg.
Kipindi hicho kilistahili kuanza Jumapili hii lakini waandaaji wa wa kipindi chenyewe wameamua kuahirisha uzinduzi huku wakitafuta sehemu nyingine ya kupeperushia kipindi hicho.
Hakuna aliyejeruhiwa kwenye mkasa huo wa moto na kilichousababisha bado hakijajulikana kwani uchunguzi untarajiwa kufanywa.
Washiriki katika kipindi hicho kutoka nchi 14 Afrika watakuwa wanashiriki katika makala ya 9 ya kipindi hicho.
Kipindi chenyewe kinatarajiwa kupeperushwa kwa siku 99 kabla ya mshindi kutangazwa.
Mshindi wa mwaka huu anatarajiwa kupokea kitita cha dola 300,000 kima sawa na kile kilichotolewa kwa mshindi mwaka 2013.
Waandalizi wa kipindi hicho Endemol na M-Net walisema kuwa juhudi za kupata sehemu mbadala ya kuendeshea kipindi hicho itakuwa kazi ngumu kutokana na ukosefu wa teknolojia inayohitajika kuendeshea kipindi hicho kwani haipatikani kwa urahisi.
''Kila juhudi italenga kupata ufumbuzi haraka iwezekanavyo kuhakikisha kuwa kipindi hicho ambacho hutazamwa na watu wengi zaidi Afrika kitaendelea.''waliongeza kusema waandalizi.
Waandalizi pia walisema kuwa washiriki kutoka Ghana walipata tatizo la viza na hivyo wakaamua kuchua raia wa Ghana wanaoishi nchini Afrika Kusini kwenyewe.
Pia washiriki wapya walitarajiwa kutoka Rwanda na Sierra Leone kwa mara ya kwanza lakini kutokana na changamoto za hapa na pale hawataweza kushiriki.
Kipindi cha Big Brother ni kipindi maarufu sana Afrika kutokana na kupendwa sana kwake, na kilianza kupeperushwa mwaka 2003. Washiriki kutoka Tanzania, Angola, Nigeria, Namibia, Zimbabwe na Afrika Kusini wamewahi kushinda katika makala ya awali.
Mnamo mwaka 2010, kipindi hicho kiligonga vyombo vya habari baada ya mshiriki mmoja kutimuliwa kutoka katika nyumba hiyo baada ya kumpiga makonde mshindani mwanamke.