.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo AJALI. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo AJALI. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 11 Septemba 2014

10 PICHAZ: AJALI YA BASI LA RUKSA YAUA WAWILI NA KUJERUHI 65 KIGOMA!

Basi la Ruksa aina ya Scania lenye namba za usajili T 273 ACX llililokuwa ikitokea mkoani Kigoma kwenda wilayani Kahama mkoani Shinyang'a likiwa limepata ajali katika kijiji cha Kanyonza wilayani Kakonko,mkoani Kigoma ambapo watu Wawili walipoteza maisha papo hapo na wengine 65 kujeruhiwa katika Ajali hiyo ya Septemba 08,2014,majira ya saa Sita mchana.
Pichani juu na chini ni Jeshi la polisi wilaya ya Kakonko lilifika eneo hilo na kuwachukuwa waliojeruhiwa  na kuwapeleka katika hospitali ya wilaya  kwa ajili ya matibabu.
 Pichani ni Baadhi ya Majeruhi wa ajali hiyo wakiwa wodini  katika hospitali ya wilaya ya Kakonko kwa ajili ya matibabu.
 Taswira ya Basi hilo la Ruksa likiwa eneo la Ajali ambapo mashuhuda wanasema chanzo cha ajali kilisababishwa na mwendo kasi.

Jumatano, 10 Septemba 2014

AJALI: Basi la Super Feo Lagonga mti na Kupinduka huko Songea….Wawili wafariki dunia, 30 wajeruhiwa vibaya


Watu wawili wamepoteza maisha huku wengine wakijeruhiwa baada ya ajali mbaya iliyotokea leo  katika  eneo la  Sanangula nje kidogo ya mji wa Songea mkoani Ruvuma ikilihusisha basi la Super Feo linalofanya safari zake kati ya Songea – Makambako lililoacha njia na kugonga mti.
BASI Chanzo cha ajali hiyo kinadaiwa kuwa ni mwendo kasi.
 
 
 

Jumanne, 9 Septemba 2014

SIO BURE LAZIMA KUNA MKONO WA MTU... AJALI NYINGINE YAUA JANA HUKO MKOANI SINGIDA




Wananchi wakishuhudia lori la saruji lililopinduka na kuua dereva wake leo eneo la Milima ya Sekenke mkoani Singida.



Pichani juu na chini malori mengine ya mizigo yakipita karibu na eneo la tukio.


Moja ya lori likitoa msaada wa kulivuta lori lililopata ajali kutoka bondeni.
DEREVA wa lori lililokuwa limebeba saruji kutoka jijini Dar es Salaam kuelekea Mwanza leo amefariki dunia baada ya lori hilo kupinduka eneo la Sekenke mkoani Singida. Watu wengine wanne waliokuwa kwenye lori hilo wamejeruhiwa.
Mmoja wa mashuhuda wa ajai hiyo ameiambia tovuti hii kuwa chanzo cha ajali hiyo ni kufeli breki kwa lori hilo lililokuwa likishuka Milima ya Sekenke na mpaka anaondoka eneo la ajali hiyo bado dereva (marehemu) na mmoja wa watu waliokuwemo aliyekuwa hai walikuwa bado wamenasa kwenye lori hilo.